logo

NOW ON AIR

Listen in Live

PATANISHO: Mume wangu alizaa na rafiki yangu

PATANISHO: Mume wangu alizaa na rafiki yangu

image
na

Habari02 October 2020 - 03:40
Bwana Nahashon aliomba apatanishwe na mkewe bi joyline akisema kuwa walikosana na mkewe na akaondoka huku akimuachia watoto.

Mke wangu ilifika mahali akaanza kuwa rude, akaanza kubishana nami na hata maji hakuwa ananipelekea bafuni. Hapo tukabishana na nikampa fursa akapumzike nyumbani.

Katika harakati Ile nilipata mwanadada mwingine lakini alikuwa anatesa watoto wangu na pia Hana usafi lakini tulitengana.

Nahashon anasema heri mke wa Kwanza ambaye wametoka mbali na ambaye anapenda kuliko mwanamke mwingine.

Alipopigiwa simu bi Joyline alikata simu pindi tu aliposkia yupo hewani, mara ya pili alisema kuwa kamwe hataki kuongea na mumewe.

"Sasa sijui nitasemaje labda ameogopa na yeye huogopa kuongea na watu. Hawa watoto bado ni wake na kuna vile vitu wanaweza kosa kutoka kwa mama mzazi." Alisema Nahashon.

Joyline alisema,

"Siwezi rudi sahizi kwani hawezi badilisha tabia na umuulize huyu ni mke wa ngapi? Leo huwa mzuri kesho anabadilika na mipango zake za kando ndio zilifanya nibadilike."

Aliongeza, nilikuwa na rafiki baadaye alimchukua akamleta kwa nyumba yangu, akanifukuza na wakabaki naye. Isitoshe alizaa na rafiki yangu." Alipopewa fursa ya kujitetea, Nahashon alisisitiza kuwa mwanadada huyo sio rafiki yake na mtoto huyo sio wake kwani vipimo vya DNA vilithibitisha.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved