Runinga ya Citizen ambayo ilifichua uhalifu huo uliobandikwa jina "Westlands undercover" ulidai kwamba maafisa katika idara ya uhamiaji na mashirika mengine ya usalama wa serikali walipanga kufukuza familia moja ya kihindi ili waweze kunyakua mali ya familia hiyo.
Muchiri alizidi kueleza kuwa yeyote yule pamoja na runinga ya Citizen aliye na ushahidi kuhusu suala hilo, wanaweza kufikisha ripoti hiyo kwa mkurugenzi wa kitengo cha mambo ya ndani.
Wanaweza pia kuwasilisha ushahidi huo kwa huduma ya kitaifa ya polisi, Charlton Muriithi ambaye anaweza kufikiwa kwa nambari 0798474619 au barua pepe: @nationalpolice.go.ke
Katika ufichuaji huo, kulikuwa na mpango ambao ulikuwa umepangwa vizuri kwa malengo ya kumfukuza mfanyibiashara huyo na dadake.
Ufichuaji huo ambao ulieleza na kuweka mambo wazi kuwa wahusika hao walikuwa na lengo la kuondoa familia hilo humu nchini ili wabadilishe umiliki wa mali inayomilikiwa na Dilip Bakrania na dadake Hansa Bakrania.