logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Je atawahi? Kipchoge ateuliwa kwa tuzo la mwanariadha bora wa mwaka

Je atawahi? Kipchoge ateuliwa kwa tuzo la mwanariadha bora wa mwaka

image
na

Habari02 October 2020 - 03:46
Kipchoge-hugging-his-wife
Bingwa wa dunia wa mbio za marathon Eliud Kipchoge na bingwa wa dunia wa mbio za mita 1500 Timothy Cheruiyot wameteuliwa kwa tuzo la mwanariadha bora wa mwaka wa IAAF.

Kuteuliwa kwake Kipchoge kumejia siku kadhaa tu baada ya kuandikisha historia kama binadamu wa kwanza kukimbia na kumaliza mbio za nyika chini ya masaa mawili.

Kipchoge na Cheruiyot ni miongoni mwa wanariadha 11 walio kwenye orodha iliyotolewa na IAAF kwa hafla hiyo ya kila mwaka itakayoandaliwa November tarehe 23 jijini Monaco, Ufaransa.

Wawili hao watakabiliwa na ushindano mkali kutoka kwa wamarekani Donavan Brazier, Christian Coleman na Noah Lyles.

David Rudisha ambaye ndio bingwa wa mita 800 na anayeshikilia rekodi ya mbio hizo na bingwa mara mbili wa olimpiki, ndiye mkenya pekee amewahi shinda tuzo hizo.

Rudisha alituzwa mwaka wa 2010.

Upigaji kura wa mwanariadha bora wa kiume utafungwa Novemba tarehe 4. Baadae wanaume na wanawake 5 watatangazwa na shirika la riadha duniani, IAAF.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved