logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uchaguzi Kibra: Imran Okoth apata ushindi, Mariga ampa kongole

Uchaguzi Kibra: Imran Okoth apata ushindi, Mariga ampa kongole

image
na

Burudani02 October 2020 - 04:02
Imran okoth
IEBC imemtangaza rasmi Imran Okoth wa ODM kuwa mshindi wa uchaguzi mdogo wa Kibra. Okoth alipata kura elfu 24,636, akifuatiwa na mwaniaji wa Jubilee McDonald Mariga aliyepata kura 11,230.

Eliud Owalo wa ANC alipata kura elfu 5,275.

Wakati huo huo Mariga amekubali kushindwa. Akimpa kongole mpinzani wake wa karibu Imran Okoth, Mariga anasema ameridhishwa na jinsi uchaguzi huo ulivyoendeshwa.

Ushindi wa mwaniaji wa ODM Imran Okoth katika uchaguzi wa Kibra haufai kuwagawanya wakaazi wa eneo hilo. Viongozi wa ODM Ochillo Ayacko na Mohamed Sumra wanasema ingawaje kulikua na makosa ya uchaguzi, chama chao kinajitahidi kuheshimu maridhiano na uiano.

IEBC imetakiwa kujitahidi zaidi katika kuhamasisha watu kuhusu umuhimu wa kujitokeza wakati wa chaguzi ndogo. Mkurugenzi wa shirika la HAKI Africa Hussein Khalid anasema katika chaguzi hizo chini ya nusu ya idadi ya watu hujitokeza kupiga kura. Pia anataka adhabu kali kutolewa kwa wanaojihusisha na makosa wakati wa uchaguzi.

Tumejaribu sana katika chumba cha kulala cha ODM. Haya ni matamshi ya wabunge wa Jubilee Kimani Ichungwa, Nixon Korir na John Kiarie ambao wamempongeza mwaniaji wao McDonald Mariga kwa kushindana vyema katika uchaguzi huo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved