Masaibu ya Babu Owino, ataja sababu za mahasidi kutaka kumtoa uhai

Babu+pic
Babu+pic
Mbunge wa Embakasi Mashariki Babu Owino amepiga taarifa katika kituo cha polisi na kuandikisha kauli kuwa maisha yake yapo hatarini.

Babu amesema kuwa kuna watu asiowajua wanaotaka kumtoa uhai.

Kulingana na mwanasiasa huyu shupavu, gari aina ya Saloon inamfuata aendapo na hivi anahofia sana kuwa kuna njama ya kumuangamiza.

 “Kwa kipindi cha miezi miwili sasa nimekuwa katika hali sio nzuri ya kutupiwa cheche za matusi na vitisho kutokana na aina ya siasa ninazofanya..."

"Najulikana kwa kuwatetea watu wa kawaida bila woga.Jambo hili linaonekana kuwakera watu wenye mamlaka makubwa visivyo...," kipande cha kauli kiliandikwa.

 Babu amesema kuwa ataendeleza juhudi zake za kuwatetea wanyonge hadi Mungu amtoe uhai.

"Na nikimaliza,sitakoma. Lazima mauti yamkute kila mtu na siku yangu itafika.Siogopi kufa kwa kile ninachokiamini na kuwatumikia watu wangu. Tialala!"

Owino amevitaka asasi za usalama na Inspekta jenerali wa polisi Hillary Mutyambai kuzidisha juhudi katika za kuchunguzi kisa hicho.