Jamaa huyu alipiga simu katika kipindi cha Mbusi Na Lion TekeTeke na kusema kuwa anaweza kutaja wanandoa wasiofanya tendo la ndoa.
"Eeh naweza kujua watu ambao hawajatamba ama wametamba (Kushiriki ngono)..."
Jamaa huyu aliwashangaza Mbusii Na Lion kwa kusema kuwa anafahamu siri nyingi za familia.
Watu wanaokimbia usiku wametajwa sana kuwa na chimbuko la Magharibi mwa Kenya.
Jamaa hawa wana uwezo wa kukimbia kwa giza bila kuonekana.
Iwapo watapatikana wanaweza toa chochote ili kujinusuru.
Watu hawa wana sifa za kusumbua watu wanapolala nyakati za usiku.
Akifungukia kitengo cha Toboa Siri, jombi huyu alisema kuwa mbio zake ni sawa na za mkimbiaji na nyota wa ridha Usain Bolt.
"Ata Usain Bolt hawezi kuniacha....' Aliisimulia Toboa Siri
Kipindi hiki huwa kinaruka kila siku (Jumatatu- Ijumaa) hadi saa moja kamili.