logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(+Video )Benjamin Washiali ajitetea kuhusu video aliyopiga mtu

(+Video )Benjamin Washiali ajitetea kuhusu video aliyopiga mtu

image
na

Habari02 October 2020 - 04:38
HfvTzy5LI8DghxCIvXUAETK2d
Mbunge wa Mumias mashariki Benjamin Washiali amekanusha taarifa zilizokuwa zikisambaa kuwa alimpiga na kumjeruhi kijana barobaro kwenye video inayosambaa kama moto jangwani.

Kipande hicho kifupi cha video hiyo kinamwonyesha Mbunge Benjamin Washiali akimchapa mwanamume mwingine.

https://twitter.com/amerix/status/1213850734502010881

Washiali anaonekana akimshambulia kwa ngumi na mateke.

Benjamin amejitetea kuwa tukio hilo lilifanyika mwaka wa 2015 na jamaa anayemchapa alifumaniwa akiiba mafuta.

Watumiaji wa mitandao ya kijamii walijawa na hamaki huku wakimtaka Washiali kujiuzulu.

"Hii ni video ya zamani mwaka 2015, sio ya sasa. Nilijawa na ghadhabu baada ya kumpata mwanamume mmoja akivuja mafuta kutoka kwa moja ya trekta inayohudumu katika shamba moja la miwa," alijitetea mbunge huyu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved