Mwakilishi mmoja wa bunge la kaunti ya Kiambu ameaga dunia akiwa katika ziara ya kikazi nchini India . mwakilishi huyo wa wadi ya kahawa Wendani Cyrus Omondi ameriotiwakuaga dunia baada ya kukumbwa na mshutuko wa Moyo ,amesema spika wa bunge la kaunti hio Stephene Ndichu .
Ndichu amesema mwakilishi huyo ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya unge la kauti kuhusu elimu alikuwa na wenzake wakati wa warsha kuhusu ya elimu alipofariki katika chumba chake .
Omondi, alikuwa kiongozi mchangamfu ambaye alishindatiketi ya jubilee ili kuliwakilisha eneo hilo licha ya kuwa ni mwenyeji wa Kauti ya Siaya na kufaulu kushinda kiti katika kaunti yenye idadi kubwa ya watu wa jamii ya kikuyu .
Kifo chake kimewatamausha wengi kwani inaripotiwa kwamba alikuwa katika hali nzuri ya kiafya . Wenyeji walikuwa walimwita kwa majina ya utani ‘Cyro’ au ‘Gearbox’.