logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Picha ya siku: Jamaa afunga harusi akiwa amevalia sare ya Arsenal

Picha ya siku: Jamaa afunga harusi akiwa amevalia sare ya Arsenal

image
na

Burudani02 October 2020 - 09:55
Jamaa mmoja amewashangaza wengi na kufurahisha wengine baada ya kuchapisha picha zake na mkewe mtandaoni, baada ya kufunga harusi.

Kilicho shangaza na kufurahisha ni kuwa kinyume na bwana harusi wengi ambao huvalia suti, yeye aliamua kuadhimisha siku hiyo akiwa amevalia sare za Arsenal.

Ni dhahiri kuwa jamaa huyo ni shabiki sugu wa Arsenal na licha ya timu hiyo kuwa na msimu mbaya, aliamua hilo halitamzuia kufurahia harusi yake na timu anayoipenda.

Isitoshe alihakikisha kuwa amevalia sare ya Arsenal ya nyumbani (nyekundu) na ya ugenini (njano)

Alichapisha picha zile na ujumbe uliosema; I Love you home & away (Nitakupenda nyumbani na mbali na nyumbani au ugenini). Kisoka, timu zote duniani lazima zicheze mechi dhidi ya mahasimu wao, nyumbani kwao na pia ugenini.

Tazama picha zifuatazo;


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved