logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Tumezuiwa kuingia kwa kaburi la bwanangu.." Mkewe bilionea Reginald Mengi alia

"Tumezuiwa kuingia kwa kaburi la bwanangu.." Mkewe bilionea Reginald Mengi alia

image
na

Habari02 October 2020 - 05:15
reginald mengi
Reginald Mengi ni bilionea kutoka Tanzania na ambaye aliaga dunia mwaka uliopita huku akimuacha mke, Jacqueline Mengi na watoto wawili.

Hapo awali, Jacqueline Mengi alikuwa msanii aliyetambulika kwa jina K-Lynn.

Jacqueline amewashangaza wengi pale alipofunguka na kukiri kuwa anazuiwa kutembelea kaburi la mumewe.

Kupitia mtandao wake wa Twitter, aliandika;

Nimenyamaza kwa mengi sana tu. Mmefikia hatua ya kunizuia mimi na wanangu kuingia kwenye kaburi la mume wangu, tunafukuzwa eti mpaka tuombe ruhusa ya kuingia kwenye kaburi la mume na Baba wa watoto wangu! Nimechoka, sitakubali kuendelea kuona wanangu wakisononeka na sitakaa kimya.

Mumewe bwana Mengi, aliaga dunia mnamo taraehe 2, Mei, 2019 akiwa na umri wa miaka 75.

Alikuwa tajiri mkuu aliyemiliki kampuni kadhaa za uanahabari pamoja na kampuni zingine Tanzia kote.

Mengi pia alikuwa mwandishi na aliandika kitabu kwa jina, I can, I will, I must.

Kabla ya kumuoa Mengi, bi Jacqueline aliwahi shinda taji la Miss Tanzania. Anajulikana kwa ngoma zake "Crazy over you, "Nalia kwa furaha " na nyinginezo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved