Makamu wa rais wa taifa la Iran Masoumeh Ebtekar, ambaye pia anasimamia masuala ya wanawake na familia amepatikana na virusi vya Corona . Makamu huyo ambaye pia anajulikana kama msemaji wa kiingereza wa watekaji nyara wa mwaka wa 1979 katika ubalozi wa Amerika nchini humo na kusababisha mgogoro wa kidiplomasia uliodumu siku 444 alipimwa na kupatikana na daalili za virusi hivyo .
Siku ya jumanne maafisa wa Iran walithibitisha kwamba naibu waziri wa afya Iraj Harirchi alikuwa pia ameambukizwa virusi vya corona na aliwekwa katika wadi ya kutengwa kwa uangalizi .
Taifa hilo limefutilia mbali mahubiri ya siku ya ijumaa katika mji mkuu Tehran na kote nchini . hatua hiyo imechukuliwa baada ya ongezeko la haraka na la kuhofisha la watu walioambukizwa kutoka idadi ya watu 100 hadi watu 246 huku vifo 26 vikithibitishwa . Iran Pia imewapiga marufuku raia wa China kuingia nchini humo .