Siku ya jumanne maafisa wa Iran walithibitisha kwamba naibu waziri wa afya Iraj Harirchi alikuwa pia ameambukizwa virusi vya corona na aliwekwa katika wadi ya kutengwa kwa uangalizi .
Taifa hilo limefutilia mbali mahubiri ya siku ya ijumaa katika mji mkuu Tehran na kote nchini . hatua hiyo imechukuliwa baada ya ongezeko la haraka na la kuhofisha la watu walioambukizwa kutoka idadi ya watu 100 hadi watu 246 huku vifo 26 vikithibitishwa . Iran Pia imewapiga marufuku raia wa China kuingia nchini humo .