logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ni kubaya! VP wa Iran aambukizwa virusi vya Corona .

Ni kubaya! VP wa Iran aambukizwa virusi vya Corona .

image
na

Habari02 October 2020 - 09:52
IRAN VP
  Makamu wa rais wa taifa la Iran Masoumeh Ebtekar,  ambaye pia anasimamia masuala ya wanawake na familia  amepatikana na virusi vya  Corona . Makamu huyo ambaye pia anajulikana kama  msemaji wa kiingereza wa watekaji nyara wa mwaka wa 1979 katika ubalozi wa Amerika nchini humo  na kusababisha mgogoro wa kidiplomasia uliodumu siku 444  alipimwa na kupatikana na daalili za virusi hivyo .

Siku ya jumanne maafisa wa Iran walithibitisha kwamba  naibu waziri wa afya Iraj Harirchi  alikuwa pia ameambukizwa virusi vya corona na aliwekwa katika wadi ya kutengwa  kwa uangalizi .

Taifa hilo limefutilia mbali mahubiri ya siku ya ijumaa  katika mji mkuu Tehran  na kote nchini . hatua hiyo imechukuliwa baada ya ongezeko la haraka na la kuhofisha la watu walioambukizwa kutoka idadi ya watu 100 hadi watu 246 huku vifo 26 vikithibitishwa . Iran Pia imewapiga marufuku raia wa China kuingia nchini humo .


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved