logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ufisadi si jambo geni Kwa taasisi za Kenya!, Maafisa wanne wa KEBS watiwa mbaroni

Ufisadi si jambo geni Kwa taasisi za Kenya!, Maafisa wanne wa KEBS watiwa mbaroni

image
na

Habari02 October 2020 - 07:22
KEBS
Maafisa wanne wa halmashauri ya kutathmini ubora wa bidhaa nchini KEBS wametiwa mbaroni kutokana na ufujanji wa shilingi milioni 12.Wanne hao ni miongoni mwa maafisa wengine saba kutoka kaunti ya Kisumu ambao wanashutumiwa kwa kuiba hela hizo..

Maafisa hao ambao wamezuiliwa na idara ya ujasusi nchini DCI wanatarajia kufikishwa mahakamani hapo kesho kujibu madai ya wizi wa pesa za umaa.

Waliotiwa mbaroni ni Jacqueline Njeri Kangiri ambaye ni Meneja mkuu wa KEBS kaunti ya KIsumu japo akahamishwa hadi Nairobi ,Catherine Nangila Wanyonyi ambaye alikuwa nafanya kazi katika idara ya kutathmini biashara eneo la Kisumu na wote kutiwa mbaroni Ijumaa.

Wengine ni Linet Bitengo Nyanchama na Daniel Ambrose osumba ambao wote walikuwa wahasibu wa pesa.

Wanne hao sasa watafikishewa katika mahakama za Kisumu kujibu madai ya ufisadi dhidi yao hya kuiba shilingi milioni 12 walipokuwa wanahudumu katika matawi ya KEBS kaunti ya Kisumu kati ya mwaka 2017 na 2018..

DCI sasa imeanza mcahkato wa kuwatafuta watu wengine watatu ambao wanakumbwa na madai sawia akiwemo Erick Kibet Sawe ,Rose Wangui Gacheru  na Florence Awino Ouma,wote waliokuwa wanafanya kazi kjatika halmashauri hiyo kaunti ya Kisumu.

Kwa pamoja watu hao saba wanatuhumiwa kewa kuiba shilingini milioni 12,791,126 kutoka kwa za KEBS .


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved