logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Maafisa 8 wa polisi wanusurika kifo baada ya kambi yao kuteketezwa Naivasha

Maafisa 8 wa polisi wanusurika kifo baada ya kambi yao kuteketezwa Naivasha

image
na

Burudani02 October 2020 - 07:48
h9MMVvNf.jfif
Maafisa wanane wa polisi wamenusurika kifo baada ya kambi yao kuteketezwa eneo la Naivasha wakati wa mandamano ya kukashifu udhalimu wa polisi.

Kisa hicho cha Alhamisi, Juni 11 asubuhi, kiliwashuhudia maafisa hao wakipoteza mali yenye thamani ya pesa.

Kulingana na wakazi, waliotekeleza kitendo hicho walianza kwa kufungia nje mlango wa afisa aliyekuwa zamuni kabla ya kuwasha gurudumu nje ya mlango wake.

Moto huo ulianza kusambaa katika nyumba zingine huku maafisa hao wakihangaika kutorekea usalama wao, moto huo ukichukua masaa mawili kuzima.

"Walikuwa wanalenga nyumba ya Inspekta ambaye hakuwepo lakini moto huo ulichoma nyumba yake kabla ya kusambaaa kwa nyumba zingine," alisema mkazi mmoja.

Inaaminika kuwa wakazi wa eneo hilo wamekuwa wakilalamikia kudhulumiwa na maafisa wa polisi wa kambi hiyo jambo ambalo linasemekana lilichangia tukio hilo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved