logo

NOW ON AIR

Listen in Live

D-Day :Waiguru kujua hatima yake leo

D-Day :Waiguru kujua hatima yake leo

image
na

Yanayojiri02 October 2020 - 08:56
Juhudi za kumuokoa gavana wa kirinyaga Anne Waiguru zinaanza leo  anapojitayarisha kujitetea mbele  ya senate .

Gavana huyo amejipata matatani kisiasa wakati ambapo washirika wakuu kisiasa wanazingatia uwezekano wa kumnasua ingawaje hatua hiyo itakuwa pia na athari zake.

Leo senate itaamua  iwapo gavana huyo atasikizwa na jopo la wenzao 11 au maseneta wote.

Pamezuka mirengo miwili katika senate kati ya wanaotaka kumuokoa Waiguru ambao ni  maseneta wa mrengo wa rais Kenyatta na kiongozi wa ODM Raila Odinga na wanaompinga  gavana huyo walio katika mrengo wa tanga tanga unaomuunga mkono naibu wa rais William Ruto.

Baada ya kuondolewa kwa washirika wa Ruto kutola uongozi wa seneti huenda Waiguru ana nafasi ya kuweza kujiokoa kutoka shoka la kuondolewa afisini lakini hilo litathibitika tu wazi siku zijazo. Tayari chama cha ODM kimesema kitalenga kumtetea Waiguru asalie afisini


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved