logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Vurugu zashuhudiwa katika bunge la kaunti ya Kitui wakati wa kujadiliwa kwa mswada wa kumtimua gavana

Vurugu zashuhudiwa katika bunge la kaunti ya Kitui wakati wa kujadiliwa kwa mswada wa kumtimua gavana

image
na

Habari02 October 2020 - 08:14
ngiluu
Vihoja vimeshuhudiwa mapema hii leo katika bunge la kaunti ya Kitui baada ya mawakili wanaomwakilisha gavana Charity Ngilu kutimuliwa na wawakilishi wadi wa kaunti hiyo.

Mapema hii leo, mawakili hao walikuwa wamezuiliwa kuingia katika bunge hilo hatua ambayo waliitaja kuwa kinyume na sheria.

“You cannot lock us out of a public office, huku si kwa mamayako ama babayako, tell the speaker to give us as letter of cancellation, you invited us, no one is getting into this office if you do not allow us in,” Wakili Morris Kimuli .

Kulinmgana na mawakili hao, walikuwa wameenda katika bunge hilo kumwakilisha gavana ambaye alikuwa ameagizwa kufika mbele yake.

MCAs walikuwa wamemtaka Ngilu kufika mbele ya bunge hilo siku chache tu baada ya mahakam ya kuu kusitisha mchakato wa kutimuliwa.

Mawakili hao Morris Kimuli na Martin Oloo walikuwa wamejihami na faili za ushahidi huku taarifa zikidai kuwa Kimuli alijeruhiwa wakati wa vurugu hizo.

Wakili huyo sasa yuko katika hospitali kuu ya Kitui huku mwenzake akilazimika kuandikisha taarifa katika kituo cha polisi cha Kitui.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved