logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watoto 4 waliouawa na mama yao wazikwa

Watoto 4 waliouawa na mama yao wazikwa

image
na

Habari02 October 2020 - 08:18
funeral
Wakaazi wa Kinangop hatimaye wamezika watoto wanne walioangamizwa na mama yao mzazi wiki ililyopita.

Watoto hao Melody Warigia (8 ), Willy Macharia (6), Samantha Njeri (4 ) na  Whitney Nyambura (2 ), wamezikwa hii leo katika kaburi la pamoja.

Hotuba ya waathiriwa ilikuwa imeandikwa kwa ufupi kama njia ya kuonyesha kuwa maisha ya watoto hao yalikatizwa kighafla

 “The late met her death on the night of Friday, June 26 under unclear circumstances, shine all the way in the land of the living untill we meet again, rest in peace.”

Mshukiwa mkuu na ambaye ni mama yao mzazi Beatrice Mwende alisema kilichomfanya kuwauwa watoto hao ni shetani na mpenziwe wa zamani.

Akiwa mbele ya mahakama ya Naivasha, mwanamke huyo wa miaka 42 aliomba mahakama kumuonea huruma ila akasema yupo radhi pia kufungwa gerezani.

Mwanamke huyo alisema kuwa siku ya kutekeleza uovu huo alishikwa na mapepo chanzo ambacho kilimpelekea kutekeleza tukio hilo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved