logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uhuru ahamia Jumba la Harambee kutoka Ikulu kwa ajili ya COVID 19

Uhuru ahamia Jumba la Harambee kutoka Ikulu kwa ajili ya COVID 19

image
na

Burudani02 October 2020 - 08:20
Statehouse
  Rais Uhuru Kenyatta  amehamia jumba la Harambee baada ya ikulu kufungwa wafanyikazi wanne walipopatikana na virusi vya corona .

Rais Kenyata  amesema hajapatikana na virusi hivyo na amekuwa akifanya kaz katika jumba la Harambee  iliyotajwa kuwa salama .wafanyikazi wake pia wamehamia jengo hilo naye .

Rais Kenyatta amekuwa akifanyia kazi Ikulu ya Nairobi hadi  visa vya corona vilivporipotiwa Juni tarehe 15 katika makao hayo yake .mikutano yake yote sasa  imekuwa ikifanyika Harambee .

Kabla ya visa hivyo vya corona kuripotiwa Ikulu rais alikuwa akiandaa mikutano  yake  yote  ikiwemo na wabunge  na baadhi ya wanasiasa katika Ikulu .


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved