Msando alielekezwa katika kifo na wandani wa IEBC- Roselyn Akombe

Aliyekuwa kamishna wa tume ya uchaguzi na mipaka  Roselyn Akombe  amesema kwamba   maneja wa ICT aliyeuwa wa tume hiyo Chris Msando  aliongozwa kwenda kuuawa na watu waliokuwa wakifanya kazi katika tume ya IEBC.

Amesema yuko tayari kutoa ushahidi mbele ya jopo la kuchunguza mauaji ya Msando iwapo kunayo  huku akiwalinganisha waliotekeleza mauaji hayo kama   Judas Iscariot.

Akombe amesema kwamba maamlaka haziko tayari kukamatwa waliomwua msando hukuakiishtumu afisi ya mkurugenzi wa mashataka ya umma kwa kujikokota kuhusiana na kesi hiyo .

Siku hii miaka mitatu iliyopita  mwili wa msando ulipatikana katika msitu wa Muguga huko Kikiyu  katika tukio ambalo nusura lisambaratishe uchaguzi wa agosti tarehe nane mwaka wa 2017, wiki moja kabla ya kuandaliwa .

Alikuwa ameteswa na kulikuwa na majeraha katika mgongo na mikono yake  kwani waliomwua walitaka awape  password ya mfumo wa kupeperusha matangazo ya uchaguzi .uchunguzi wa mwili wake ulionyesha tu kwamba alikuwa na majeraha ya kukatwa lakini baadaye ilibainika kwamba alinyongwa .

Msando  alikuwa ameahidi kuhakikisha kwamba uchaguzi huru na wa haki unafanyika na mfumo uliokuwa umetumie haungeweza kudukuliwa kwani ni yeye pekee aliyekuwa na password ya mfumo huo .Ushindi wa rais kenyatta baadaye ulitupiliwa mbali na mahakama ,ingawaje alishinda uchaguzi  wa marudio ambao upinzani ulisusia .

Akombe, kupitia msururu wa jumbe za twitter  ameiweka IEBC katikati ya mauaji ya Msando  akisema wenzake ndio waliomsaliti kwa waliotekeleza mauaji yake  .amesema yuko tayari kusema anachofahamu .

Alitorokea Marekani akihofia usalama wake  na akarejea kulifanyia kazi shirika la umoja wa mataifa nchini humo .

“… Ni uchungu  kwamba  siku kama hii miaka mitatu iliyopita  wenzako walikupeleka kichinjio .kama Judas  walikuuza kwa senti 30’ Akombe aliandika katika twitter .

“ Tutahakikisha tunapigania haki yako na tuipate  hata iwe muda gan’ alizidi kuandika .

Lakini  mwenyekiti wa IEBC wAfula Chebukati amesema  sio haki kwa Akombe kuzungumza sasa  miaka mitatu baadaye ilhali alikuwepo wakati  Mauji hayo yalipotendeka .

" Sote tunataka kuona haki ikitendeka  kwa familia ya Msando  .tumesema hilo kuanzia mwanzo’ Chebukati aliliambia gazeti la The Star

Akombe  anaafa kuzisaidia maamlaka kufahamu ukweli kuhusu mauaji ya Msando .

" Yaonekana kuna jambo analofahamu ambalo wengine hatujui .Naamini hili linafaa kutoa habari za kutosha kwa idara za uchunguzi .Labda huenda habari hizo zitasaidia kukamilishwa kwa uchunguzi’ Chebukati amesema

Ameongeza kwamba  IEBC imekuwa ikifanya kila jambo inaloweza kupata ukweli kuhusu mauaji ya Msando .

Chebukati amesema iwapo Akombe hawezi kujiwasilisha kwa  DCI basi mipango inaweza kuwekwa ili  maelezo yake yachukuliwe akiwa Marekani .

Akombe amekishauri chama cha wanasheria nchini LSK kuchukua kesi hiyo na kuifikisha kortini kwa maslahi ya umma na yuko tayari kutoa ushahidi .

Lakini Rais wa LSK Nelson Havi amepuuzilia pendekezo hilo .

“ Mimi ni DCI? Sifanyi uchunguzi wa mauaji.waulize watu wanaoshughulikia mambo kama hayo’ alisema