logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Askari walevi wawaua watu 13 DRC

Askari walevi wawaua watu 13 DRC

image
na

Habari01 October 2020 - 10:48
Na BBC

Askari waliokuwa wamelewa nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamemimina risasi na kuua watu 13 na wengine kadhaa kujeruhiwa.

Mmoja wa wahanga anaripotiwa kuwa mtoto wa miaka miwili.

Mauaji hayo yalitokea usiku wa Alhamisi katika jimbo la Kivu kusini mashariki mwa nchi hiyo

Jeshi la Jamuhuri ya demokrasia ya Kongo linawatafuta askari hao waliouwa watu 13, wakiwemo wanawake na watoto katika mji wa Uvira.

Makundi kadhaa ya wanajeshi pamoja na walinda amani wa Umoja wa mataifa wako katika mji huo ili kuwalinda raia.

Ni siku ya masikitiko makubwa katika fukwe za ziwa Tanganyika, kumekuwa na waandamanaji wenye hasira dhidi jeshi la Kongo katika mji wa Sange, tangu majira ya asubuhi eneo ambalo barabara nyingi zilikuwa zimefugwa.

Waandamanaji hao wanataka familia zilizoathirika kulipwa fidia na huduma za afya kwa wale waliojeruhiwa.

Jeshi limeiambia BBC kuwa askari wale walifanya tukio hilo kwa sababu walikuwa wamelewa na watafukuzwa jeshini na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Tukio hili limekuja wakati ambao mji huo bado ulikuwa unakabiliana na athari za mfuriko makubwa yaliyouwa watu 40 na wengine maelfu walipoteza makazi yao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved