logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Makumbusho ya 42 ya kifo cha hayati Mzee Kenyatta yafanyika faraghani

Makumbusho ya 42 ya kifo cha hayati Mzee Kenyatta yafanyika faraghani

image
na CONSOLATA MAKOKHA

Habari23 August 2020 - 09:00

Muhtasari


    Kinyume  na makumbusho ya miaka ya awali ambapo makumbusho ya kifo cha hayati mzee Jomo Kenyatta yalifanyika hadharani huku viongozi mbali mbali wakialikwa mwaka huu mambo yalikuwa tofauti.

    Soma habari zaidi;

    Jumamosi Agosti 22 mwaka huu ilikuwa miaka 42 tangu mzee Kenyatta kufariki na hafla ya mwaka huu ilikuwa tofauti kwani ni familia ya marehemu hayati mzee Kenyatta pekee iliyohudhuria.

    Hii pia ilikuwa mara ya kwanza rais Uhuru Kenyatta alikosa kuweka shada la maua katika kaburi la babake.

    "Kama rais, nimeshauriana na familia ya Mzee Kenyatta. Tumekubaliana kwa pamoja kwamba makumbusho haya ya 41 yatakuwa ya mwisho kufanyika kwa njia hii," Uhuru alisema mwaka jana katika hafla iliyoandaliwa katika kanisa la Holy Family Basilica, Nairobi.

    Soma habari zaidi;

    Mzee Jomo Kenyatta alifariki Agosti 22, 1978 mwendo wa saa tisa unusu asubuhi akiwa usingizini katika Ikulu ya rais ya Mombasa.


    RADIO JAMBO FREQUENCIES

    Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


    logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved