logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uhuru atuma rambirambi zake kwa Aden Duale baada ya kumpoteza mama yake

Uhuru atuma rambirambi zake kwa Aden Duale baada ya kumpoteza mama yake

image
na

Habari01 October 2020 - 09:54
Aden Duale
Rais Uhuru Kenyatta ametuma risala za rambirambi kwa familia ya mbunge wa Jiji la Garissa Aden Duale baada ya kumpoteza mama yake.

Duale alimpoteza mama yake Mama Hawa Jumanne huku rais akijiunga na waombolezaji kwa kutumba risala zake kwa famili ya mbunge huyo.

Rais alimuomboleza Mama Hawa Kosar kama mwanamke mnyenyekevu, mwenye bidii na mwenye kujitolea katika kazi za Mungu, huku akisema maneno na ushuri wake wenye maarifa utapezwa maishani.

Chama cha Jubilee pia kilituma risala za rambi rambi zao kwa familia ya Duale na kuandika ujumbe ufuatao;

"Chama cha Jubilee kinajiunga na familia ya mbunge wa jiji la Garissa Aden Duale kuomboleza kifo cha mama yake Mama Hawa Kosar Shaurie

Wacha Mungu aijaze familia hiyo na nguvu wakati huu wamekabiliwa na kifo cha mama yao,Mama Hawa Kasor lala mahala pema peponi." Ujumbe ulisoma.

Pia naibu rais William Ruto alimkumbuka mwendazake kama mwanamke wa dini aliyejitolea na amabaye alilea watoto wenye bidii.

"Rehema zetu za moyono zinawaendea familia na mbunge wa Garissa Aden Duale kwa kumpoteza mama yao mzazi, Mama Shaurie alikuwa mwanamke wa dini aliyepewa heshima na aliyekuza na kuwalea watoto wenye bidii licha ya kuwa na changamoto." Aliandika Ruto.

Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved