logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Murkomen anza kujipanga kuondoka,'Waziri Tobiko aapa kumfurusha Murkomen

'Murkomen anza kujipanga kuondoka,'Waziri Tobiko aapa kumfurusha Murkomen

image
na

Habari01 October 2020 - 09:41
tobiko
Vita za cheche za maneno kati ya seneta wa Elgeyo Marakwet Kipchumba Murkomen na waziri wa mazingira Keriako Tobiko zinazidi kuchacha na kushuhudiwa kila kuchao.

Mnamo Septemba,5,Tobiko alidai kuwa Murkomen ni miongoni mwa watu ambao wanaishi katika msitu wa Embombut na hivi karibuni atamfurusha kutoka maeneo hayo.

Pia alidai kuwa Murkomen alipinga zoezi la kuwahamisha watu katika msitu wa Mau.

Wawili hao wamekuwa kwenye cheche za maneno baada ya Tobiko kumuita Naibu Rais William Ruto kama karani tu kwenye serikali.

"Hatutakubali yale yalifanyika msitu wa Mau. Wakati watu walikuwa wakitolewa Mau Murkomen alikuwa mmoja wale wale walipinga zoezi hilo

Yeye anaisha msitu wa Embombut. Murkomen anza kujipanga kuondoka." Tobiko Aliongea.

Baada ya matamshi yake Tobiko Murkomen naye alisema kuwa hatishwi na usemi wake Tobiko huku akidai waziri huyo anataka kulipiza kizazi kwake na kwa baba yake.

"Tuna waziri ambaye ana utoto, Yaani kwa sababu ya ujumbe wa twitter ameamua kulipiza kisasi kwangu na babangu," alisema Murkomen."Aliongea Murkomen.

Je cheche hizi za maneno zitashuhudiwa hadi lini kati ya viongozi hao wawili?


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved