"... Chama chetu sio tu kuhusu ndege za kibinafssi na Slay queens na kuwatukana viongozi wengine ,tuna ajenda ya maendeleo ambayo ipo katika manifesti yetu’ Raila Jr alisema
https://twitter.com/Railajunior/status/1306088096249896965
Lakini jumatano Junior alibadilisha msimamo wake akisema huenda ujumbe wake huo ulichukuliwa vibaya akisema ;
" Ufafanuzi …kama mwanachama wa kawaida wa ODM Maoni yangu sio ya chama . Nakishukuru chama cha ODM kwa kuruhusu demokrasia na kumpa kila mtu fursa ya kutoa maoni yake’ alisema
" Maoni yangu hayamlengi kiongoi yeyote na naomba radhi kwa kutafsiriwa vibaya kwa ujumbe wangu’
Msamaha wake hata hivyo hakuchukuliwa kwa wepesi kwani watu wengi walionekana kuendelea kumkosoa wakimtaka akome kuzungumzia masuala ya chama cha ODM .
" Wewe na mjombako Oburu mnafaa kujifiche sehemu Fulani hadi mikakati yote ianze kutekelezwa .. hamwezi kufunga midomo yenu’ @RealOmbatiEdwin said.
@patroba said " Ulisema ukweli . kwa kweli chama cha ODM kinadidimia .huwezi kulinganisha ODM ya mwaka wa 2007 na ODM YA 2020 mtu Kama Sifuna runs ODM like his pit latrine."