logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Nimeambia familia yangu nikifa wanizike siku hiyo,' Akothee

'Nimeambia familia yangu nikifa wanizike siku hiyo,' Akothee

image
na

Yanayojiri01 October 2020 - 09:27
Msanii Esther Akoth almaarufu Akothee amefichua kuwa ameuliza familia yake imzike siku ambayo ataaga dunia na wala si siku ifuatayo.

Akiandika hayo kwenye ukurasa wake wa instagrama Akothee alisema kwamba hataki kupitia magumu ambayo mama yake amepitia kwa mwezi mmoja huku akingooja mke wa ndugu yake aweze kupewa heshima zake za mwisho.

Akothee aligadhabishwa na vile watu wanampigia simu aweze kutoa mchango wa mazishi yao ilhali hamna mtu mmoja ambaye ameweza kumuuliza mkewe ndugu yake atazikwa lini.

https://www.instagram.com/p/CFQxLE-nEmE/

"Watu wengine bado wananitumia jumbe na hata kunipigia niweze kuchanga kwa ajili ya mazishi yao hamna mtu yeyote ambaye ameniuliza kunipeleka kwenye mazishi wala kuniuliza mazishi yako siku gani

Wakati huu sina nguvu ya kumuangalia ndugu yangu akimteremesha mke wake kwenye kaburi sijui niweke kichwa wapi?

Kwangunmimi nikifa leo nimeuliza familia yangu inizike siku hio hio, kiwewe ambacho mama yangu amepitia kwa mwezi huu mmoja akingoja nyabondo kwa ajili ya hali ya covid siweze muona akienda kwenye mazishi

Wacha Mungu akajaze kila familia iliwapoteza wapendwa wao wakati huu mgumu." Akothee Aliandika.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved