logo

NOW ON AIR

Listen in Live

NMG yaagizwa kuitoa mtandaoni taarifa ya upekuzi ya 'Covid Millionaires'

NMG yaagizwa kuitoa mtandaoni taarifa ya upekuzi ya 'Covid Millionaires'

image
na

Habari01 October 2020 - 09:20
covid milionaires
Mahakama kuu imeagiza kauni ya NMG  Kkuondoa mtandaoni taarifa ya upekzi ya  ‘Covid-19 Millionaires’  hadi kesi iliyowasilishwa dhidi yake isikizwe na kuamuliwa .

 Katika kesi hiyo  , Megascope Ltd  iliwasilisha kesi kortini kuishtaki NMG na mwanahabari  Dennis Okari  kwa kuihusisha na  sakata katika shirika la Kemsa na hivyo basi kuiharibia jina kampuni hiyo .

Jaji  Joseph Sergon  jumatano ametoa agizo la kuitaka NMG kuindoa taarifa hiyo mitandaoni baada ya Megascope kuwasilisha ombi hilo  hadi kesi hiyo sikizwe na kuamuliwa .

 Taarifa hiyo ya upekuzi  iliwekwa Youtube na kufikia sasa ilikuwa imetazamwa mara 700,000

Wakili wa   megascope  Njoroge Regeru alikuwa ametoa ombi kwa jaji  akisema taarifa hiyo   kuslaia katika mitandao ya kijamii iliendelea kuharibu sifa za kampuni ya mteja wake . Hata hivyo ombi hilo lilipingwa na wakili wa NMG Kiragu Kimani  akisema maagizo yaliyotolewa  hapo awali kwamba wasiandike taarifa zaidi kuihusu megascope na sakata hiyo yalitosha .

Kesi hiyo itatajwa Oktoba tarehe 22 .


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved