logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sikujua kama kipindi cha Selina kitakuwa kikubwa hivi-Pascal Tokodi

Sikujua kama kipindi cha Selina kitakuwa kikubwa hivi-Pascal Tokodi

image
na

Habari01 October 2020 - 09:20
Muigizaji na mwanamuziki Nelson almaarufu Pascal Tokodi anafahamika sana kwa sauti yake na hata uigizaji wake,akiwa kwenye mahojiano muigizaji Pascal alizungumzia jinsi alipata uigizaji katika kipindi cha Selina ambacho hupeperushwa katika runinga ya maisha magic east kila juma ya wiki.
"Walikuwa wanatafuta muigizaji Nick Mutuma ambaye ni rafiki yangu aliniambia nikiwa Mombasa nikiwa kazini nilikuwa naigiza kitu fulani

Aliponipigia nilisema kama huo uigizaji ni wangu basi ni wangu na kama si wangu utapata mwingine basi, baada ya siku chache alinipigia simu akaniambia kuwa hawajapata muigizaji ambaye wanamtaka napaswa kuenda katika ukaguzi nilipoenda nilichaguliwa

Kipindi cha Selina nitahishi kukishukuru maishani mwangu, kwa maana kimenikuza na hata nimesoma mambo tofauti, sikujua wala kufahamu kama kipindi hicho kitakuwa kikubwa hivyo

katika kipindi hicho kitu ambacho nimeigiza nikajivunia ni wakati ambao nilikuwa naigiza nikilia." Alieleza Pascal.

Pascal ameshinda tuzo nyingi katika uigizaji na hata katika sanaa ya muziki, huku akizungumza hayonalidai ya kwamba wanawake wengi wanapenda sauti yake kulivyo anavyoipenda.

Muigizaji huyo pia alisema kuwa wazazi wake walimuunga mkono katika kazi yake ya uigizaji na hata kumpa msukumo mkubwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved