logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Corona ilisimamisha Reggae ya BBI,'Murkomen amjibu mbunge Opiyo

'Corona ilisimamisha Reggae ya BBI,'Murkomen amjibu mbunge Opiyo

image
na

Habari01 October 2020 - 09:15
Seneta wa Elgeyo Marakwet Kipchumba Murkomen amejibu ujumbe wake mbunge wa Ugunja Opiyo Wandayi uliosoma kuwa ni masikitiko makubwa kuwa viongozi wa serikalini wameanza kampeni za siasa mapema.

Kwa mujibu wake Murkomen alisema kuwa janga la corona lilisimamisha wimbo wa reggae wa BBI, na kuwa BBI ilibadilisha hali ya wananchi wa Kenya.

"Mikutano ya BBI iliunda hali ya humu nchini kwa muda mrefu uliopita, na kwa sababu ya corona reggae ilisimama." Murkomen Alijibu.

Usemi au majibu yake yalijiri baada ya mbunge Opiyo kusema kuwa nchi iko katika hali ya kampeni za kisiasa ambapo imesalia mwaka mmoja na nusu.

"Ni kwa bahati mbaya kuwa nchi hiko katika hali ya kampeni za kisasa karibu mwaka mmoja na nusu ili uchaguzi mkuu kutimia jambo mbaya zaidi ni kuwa wanaofanya hali hii kutendeka ni viongozi wa serikalini na kutumia pesa za walipa kodi." Aliandika Opiyo.

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved