Fahamu wanakohamia wachezaji wa timu upendazo

Michezo:Jungu zima la habari za uhamisho

mkusanyiko wa habari zote za uhamisho katika soka

Muhtasari

 

  • Kocha wa Inter Milan  Antono Conte amtaka Sergio Aguero
  • Memphis Depay  hajafutilia mbali uwezekano wa kuhamia  Barcelona mwezi januari
  • Mfaransa  Houssem Aouar, 22,  anaamini kusalia Lyon ni uamuzi ufaao

 

Yote muhimu viwanjai
Image: Yusuf Juma

 

Kocha wa Inter Milan  Antono Conte  anapanga kuwasilisha ombi la kumsaini mchezaji wa Manchester City  na raia wa Argentina  Sergio Aguero, 32, ambaye mkataba wake utatamatika mwishi mwa msimu huu

 Kilabu ya Bournemouth imekataa ofa kutoka kwa  West Ham kumsajili  mshambuliaji wa Norway  Joshua King mwenye umri wa miaka 28 kwa pauni milioni 13. Hata hivyo the hammers bado ipo katika mazungumzo na Brentford kumsaini Said Benrahma mwenye umri wa miaka 25 raia wa Algeria

 Aliyekuwa mchezaji wa  Manchester Memphis Depay  hajafutilia mbali uwezekano wa kuhamia  Barcelona mwezi januari . mshambuliaji huyo wa  Uholanzi  alisalia Lyon ili kukamilisha mwaka mmoja katika mkataba wake  lakini kilabu hiyo ya Ufaransa ina chaguo la kumuuza katika kipindi kijacho cha uhamisho

 Mchezaji mpya wa  man United Facundo Pellistri,  raia wa Uruguay mwenye umri wa miaka 18  anapanga kurejea nyumbani kwao   kwa kujiunga na kilabu ya  Penarol,  ambaypo aliondoka ili kujiunga  na Old Trafford.

Manchester City  imeamua kusalia na huduma za mlinzi wa Uhispania  Eric Garcia kwa kipindi cha msimu huu kwa sababu ana thaani ya juu kuliko pauni milioni 18 ambazo Barcelona imetoa kama ofa ya kumnunua . Garcia mwenye umri wa miaka 19  anaweza kuelekea Nou Camp  kipindi kijacho bila malipo yoyote baada ya kudinda mkataba mpya .

 Kocha wa Barcelona   Ronald Koeman  amesema mshambuliaji wa Luis Suarez, 33,  angesalia Nou Camp ili kumdhihirishia ubabe wake uwanjani badala ya kutorokea  Atletico Madrid.

 Aliyekuwa mshambuliaji wa Liverpool na  England  Daniel Sturridge, 31, anaamini kwamba kurejea kwake katoka soka sasa hakuwezi kuepukika baada ya mkataba wake na kilabu ya Uturuki   Trabzonspor  kukatizwa kwa makubaliano ya pande zote  mbili  mwezi machi  na katika siku hiyo alipokea marufuku ya miezi minne kwa kukiuka sheria za michezo ya kubashiri .

 Difenda wa  Denmark  Joachim Andersen  amesema maneja  Scott Parker alimshawishi ajiunge na  Fulham .Torino  pia imekuwa ikimmezea mate mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 .

 Kiungo wa kati  Mfaransa  Houssem Aouar, 22,  anaamini kusalia Lyon ni uamuzi ufaao baada ya kuhusishwa pakubwa na uwezekano wa kuhamia Arsenal