logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Covid-19: Visa 604 vipya vya maambukizi ya corona vyarekodiwa huku 10 wakifariki

Vile vile watu 10 hii leo wamepoteza maisha yao kutokana na virusi vya

image
na Radio Jambo

Yanayojiri14 October 2020 - 13:46

Muhtasari


•Watu 10 waaga dunia kutokana na corona

•Visa 604 vya rekodiwa nchini hii leo huku 88 wakipona

Mutahi Kagwe

Visa 604 vipya vya maambukizi ya virusi vya corona vya rekodiwa humu nchini huku idadi hiyo ikifa jumla idadi ya 42,541, hii ni kutokana na sampuli 5,832 zilizopimwa saa 24 zilizopita.

Kati ya visa hivyo vipya 583 ni wakenya huku 21 wakiwa ni raia wa kigeni, 400 ni wanume ilhali 204 ni wanawake.

Mgonjwa umri wa chini ana miezi mitano huku mwenye umr wa juu akiwa na miaka 94 amesema waziri wa afya Mutahi Kagwe.

 

Huku hayo yakijiri watu 88 wamepona virusi hivyo na kufikisha idadi jumla ya 31,428 ya watu waliopona kutokana na corona.

Vile vile watu 10 hii leo wamepoteza maisha yao kutokana na virusi vya corona na kufikisha idadi jumla ya 797 ya watu walioaga dunia.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved