logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jamaa aliyemuua mkewe akamatwa na makachero wa DCI

Kulingana na maafisa wa polisi John amekuwa mafichoni baada ya kumuua Mercy

image
na Radio Jambo

Habari17 October 2020 - 11:00

Muhtasari


  • John alumuua mkewe mnamo tarehe 13 Oktoba na kuingia mafichoni
  • Mshukiwa huyo alikamatwa na makachero wa DCI mnamo tarehe 17 Oktoba

Mshukiwa wa mauaji aliyetoroka baada ya kutekeleza kitendo hicho amekamatwa na makachero wa DCI.

John Mwangi Githaiga,34 alitiwa mbaroni katika eneo la Mathangauta na maafisa wa polisi wa DCI wa eneo la kaunti ndogo Njoro.

Kulingana na maafisa wa polisi John amekuwa mafichoni baada ya kumuua Mercy Njeri Mbatia manamo Oktoba 13.

Huku akitumia kifaa chenye makali inasemekana mshukiwa huyo alimkata shingo Mercy,23 ambaye alikuwa ni mkewe hadi kifo.

"Mwangi ambaye alimkata mwendazake kwa kifaa chenye makali akachoma kichwa, mikono miguu hadi eneo la magoti amekuwa mafichoni na atashtakiwa iwezekanavyo." Ripoti ya DCI Ilisoma.

Mapema wiki hii mshukiwa mwingine aliyemchoma mkewe alikamtwa katika eneo la Kericho alipokuwa anajaribu kutoroka.

Kulingana na ripoti ya DCI John alikamatwa na maafisa wa DCI mnamo Oktoba 17.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved