Mshukiwa wa mauaji aliyetoroka baada ya kutekeleza kitendo hicho amekamatwa na makachero wa DCI.
John Mwangi Githaiga,34 alitiwa mbaroni katika eneo la Mathangauta na maafisa wa polisi wa DCI wa eneo la kaunti ndogo Njoro.
Kulingana na maafisa wa polisi John amekuwa mafichoni baada ya kumuua Mercy Njeri Mbatia manamo Oktoba 13.
Huku akitumia kifaa chenye makali inasemekana mshukiwa huyo alimkata shingo Mercy,23 ambaye alikuwa ni mkewe hadi kifo.
"Mwangi ambaye alimkata mwendazake kwa kifaa chenye makali akachoma kichwa, mikono miguu hadi eneo la magoti amekuwa mafichoni na atashtakiwa iwezekanavyo." Ripoti ya DCI Ilisoma.
Following the murder of 23-year-old Mercy Njeri Mbatia on 13th October, 2020 by her husband, @DCI_Kenya Detectives based at Njoro Sub-County have arrested 34-year-old John Mwangi Githaiga at Mathangauta area.
— DCI KENYA (@DCI_Kenya) October 17, 2020
Mapema wiki hii mshukiwa mwingine aliyemchoma mkewe alikamtwa katika eneo la Kericho alipokuwa anajaribu kutoroka.
Kulingana na ripoti ya DCI John alikamatwa na maafisa wa DCI mnamo Oktoba 17.