logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Buriani: Aden Duale aomboleza kifo cha kakake

Hii ni miezi miwili baada ya mbunge huyo kumpoteza mama yake mzazi,

image
na Radio Jambo

Burudani18 October 2020 - 09:53

Muhtasari


  • Aden Duale aomboleza kifo cha kakake mkubwa
  • Mwendazake aliaga baada ya kuhusika katika ajali ya barabara

Aliyekuwa kiongozi wa wengi katika bunge la kitifa Aden Duale anaomboleza kifo cha nduguye aliyefariki baada ya kuhusika katika ajali ya barabarani.

Kakake mkubwa, Dubow Barre Duale, alifariki baada ya kuhusika kwenye ajali alipokuwa akisafiri kwenye barabara ya Garissa-Nairobi.

Haya yanajiri miezi miwili baada ya mbunge huyo kumpoteza mamake mzazi, ni mwaka ambao utakuwa wa majonzi na kilio katika familia ya Duale.

 

Duru zimearifu kuwa Dubow alikuwa akiendesha gari lake aina ya Toyota Harrier wakati ajali hiyo ilipotokea.

Marehemu alikuwa mwanajeshi mstaafu ambaye alikuwa amegeukia biashara na alikuwa mmoja wa wafanyibishara mashuhuri mjini Garissa.

Baada ya wakenya kuona habari hizo walitumba risala za rambirambi kwa mbunge huyo na familia yake.

Kutoka kwetu wanajambo Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

(Mhariri Davis Ojiambo)

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved