- Rais aliyasema hayo katika msururu wa ukaguzi wa miradi ya amendeleo huko Kisumu
- Rais alikuwa akiwahutubia wakaazi wa Kisumu
Rais Uhuru Kenyatta amewaacha na kicheko wakaazi wa Mji wa kisumu baada ya kusema kwamba anazingatia kupata mke mwingine kutoka mji huo .
"Nilikuwa naambia Raila hapa jameni... Sijui kama mama nyumbani ataniruhusu... Akiniruhusu labda naweza kupata mtu ambaye atakuwa ananitengenezea mambo yangu pande hii..." alisema huku akicheka .
"Ndio tuwe tukitembea ukijua kuna mahali utakuwa unakula ugali ama namna?"
Wakati wa hotuba yake siku ya alhamisi akiwa Kisumu rais alisema mwafaka wa Handshake kati yake na Raila umempa amani
Uhuru amesema miaka miwili tangu mwafaka huo ,taifa limeshuhudia ustawi mkubwa na maendeleo kinyume na iwapo hawangeamua kushirikiana .
Akimsifu bwana Odinga kwa kusimama kidete na mchakato mzima wa BBI Uhuru amesema Raila Amethibitisha kuwa kiongozi halisi taifa ambaye aliyeweka azma yake kando kwa lengo la kuisadia Kenya .
Awali rais alimwelekeza waziri wa usalama wa ndani Fred Matiangi kuhakikisha kwamba barabara ya kilomita 63 ya Kisumu-Mamboleo-chemelil-Muhoroni inakamilishwa katika kipindi cha miezi mine ijayo .
" Nitarejea hapa Aprili mwaka ujao na barabara hii inafaa kukamilishwa kufikia wakati huo’