logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uhuru azingatia kupata ‘mke’ kutoka Kisumu

Rais Uhuru Kenyatta amewaacha na kicheko wakaazi wa Mji wa kisumu  baada ya kusema kwamba anazingatia kupata mke  mwingine kutoka mji huo

image
na Radio Jambo

Habari22 October 2020 - 13:44

Muhtasari


 

  •  Rais aliyasema hayo katika msururu wa ukaguzi wa miradi ya amendeleo huko Kisumu 
  • Rais alikuwa akiwahutubia wakaazi wa Kisumu 

 

 Rais Uhuru Kenyatta amewaacha na kicheko wakaazi wa Mji wa kisumu  baada ya kusema kwamba anazingatia kupata mke  mwingine kutoka mji huo .

"Nilikuwa naambia Raila hapa jameni... Sijui kama mama nyumbani ataniruhusu... Akiniruhusu labda naweza kupata mtu ambaye atakuwa ananitengenezea mambo yangu pande hii..."  alisema huku akicheka .

"Ndio tuwe tukitembea ukijua kuna mahali utakuwa unakula ugali ama namna?"

 Wakati wa hotuba yake  siku ya alhamisi akiwa Kisumu rais alisema mwafaka wa Handshake kati yake na Raila  umempa amani

Uhuru  amesema miaka miwili tangu mwafaka huo ,taifa limeshuhudia  ustawi mkubwa na maendeleo  kinyume na iwapo hawangeamua kushirikiana .

 Akimsifu bwana Odinga  kwa kusimama kidete na mchakato mzima wa BBI  Uhuru amesema Raila Amethibitisha kuwa kiongozi halisi taifa  ambaye aliyeweka  azma  yake kando kwa lengo la  kuisadia Kenya .

 Awali rais alimwelekeza waziri wa usalama wa ndani Fred Matiangi kuhakikisha kwamba   barabara ya kilomita 63 ya Kisumu-Mamboleo-chemelil-Muhoroni inakamilishwa katika kipindi cha miezi mine ijayo .

" Nitarejea hapa Aprili  mwaka ujao  na barabara hii inafaa kukamilishwa kufikia wakati huo’

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved