logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Eric Omondi amkashifu vikali Ezekiel Mutua baada ya kumkejeli

Baada ya Eric kuona matamshi yake Ezekiel mcheshi huyo naye alimkashifu vikali

image
na Radio Jambo

Habari26 November 2020 - 06:35

Muhtasari


  • Eric Omondi amuonya Eekiel Mutua dhidi ya kutumia jina lake
  • Mutua alimuambia mchekeshaji huyo kuwa anapswa kujiheshimu kwa yale anafanya kwenye mitandao ya kijamii
eric omondi

Kwa muda sasa mchekeshaji Eric Omondi amekuwa kwenye vichw vya habari baada ya kuzindua studio yake.

Mkurugenzi wa Kenyan Film Classification Board Ezekiel Mutua alimshambulia na kumkejeli Mcheshi huyo huku akimwambia anapaswa kujiheshimu.

Baada ya Eric kuona matamshi yake Ezekiel mcheshi huyo naye alimkashifu vikali huku vita vya maneno vikishuhudiwa kati ya wawili hao.

 

Kupitia kwenye ukurasa wake Eric Omondi alikuwa na haya ya kumwambia mkurugenzi huyo;

"Dktr Ezekiele Mutua  hii ni onyo yako ya mwisho, hii sio njia ya kuhutubia rais wa bara zima  wacha kutumia jina langu kwa foleni za umma ambazo ni za bai nafuu

Sijawahi fahamu huwa unafanyanya nini ili kukimu maisha yako, haujasaidia tasnia ya burudani kwa vyovyote vile, kwa hivyo ulienda Mombasa kwa ajili ya kuhotubia wanahabari kwa ajili ya hili, si ungenipa pesa hizo niongeze kamera katika studio yangu." Eric Aliandika.

Eric alimwambia Ezekiel anapaswa kutembelea studio zake ili kuona ambayo wana andaa kwa ajili ya vijana.

"Tafadhali tembelea studio za Eric Omondi, na uone ambacho tunatayarisha kwa ajili ya kuwasaidia  vijana wetu na vipaji ambavyo vinachipuka

Usiwahi ongelelea jina langu tena,haujui wala kufahamu hadithi yangu wala kuelewa mchakato wangu."

Tasnia ya burudani humu nchini imekuwa ikibadilika kila kuchao


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved