Tangu kutangazwa kwa kifo chake Magufuli nimekosa usingizi- Kikwete

Muhtasari
  • Rais Mstaafu wa Tanzania Kikwete amsifia Magufuli kwa haya
  • Kikwete wakati akimsifia rais aliyekufa alisema anakosa maneno ya kuelezea kuondoka kwa Magufuli mapema
Image: Maktaba

Rais mstaafu wa Tanzania Jakaya Kikwete amesema moyo wake bado una maumivu kufuatia kifo cha John Pombe Magufuli.

Kikwete wakati akimsifia rais aliyekufa alisema anakosa maneno ya kuelezea kuondoka kwa Magufuli mapema.

"Alikuwa kiongozi na rais wetu. Ninakosa maneno ya kuelezea kuondoka kwake. Machi 17 ni siku ambayo sitasahau kamwe. Tangu wakati huo, nimekosa usingizi na moyo wangu una maumivu, "alisema.

 

Kikwete alisema alikuwa akikaa vizuri na ndugu zake nyumbani kwake alipopokea ujumbe kuwa Magufuli ameaga dunia.

"Niliambiwa kwamba Makamu wa Rais alikuwa atoe tangazo na alitarajiwa kuwapo. Niliiacha familia yangu ikiwa na shida bila kuwaambia kilichotokea. Nilisimama pale bila kusema huku rais wetu Samia Suluhu akitoa tangazo hilo,Ilikuwa ngumu kukubali na hadi sasa bado nina huzuni kutoka ndani," Alizungumza Kikwete.

Kifo chake Magufuli kitangazwa mnamo Machi 17 baada ya kupigna miaka kumi na shidaza moyo.

Kikwete alisema alikuwa na matumaini Magufuli atatumikia na kumaliza muhula wake wa pili na kustaafu kama alivyofanya.

"Nilitarajia atamaliza muda wake na kustaafu, aondoke kwa muda mrefu. Tulitumahi atuzike wale ambao walitumikia kabla yake kwa sababu uongozi na maono yake yalikuwa yanahitajika. Sote tumeona matunda ya uongozi wake, "Kikwete alisema.

Rais huyo mstaafu alisema anaelewa majukumu ambayo hupewa urais na wakati mwingi rais anayeketi hapati wakati na familia yake.

"Hii ndio sababu nilitumai kuwa angemaliza muda wake na kufurahiya wakati mwingine na familia yake kama mimi

 

Tumetoka mbali kwa kuwa tulihudumu kama mawaziri kwa miaka 10. Magufuli alihudumu katika utawala wangu kwa doketi tatu na alikuwa kwenye mkono wangu wa kulia kila wakati, "alisema.

Kikwete alisema alimhamisha Magufuli kutoka uwaziri kwenda kwa mwingine kwa sababu alikuwa akimfahamu kama msanii.

Kikwete alisema haya wakati wa hafla ya mazishi ya Magufuli siku ya Ijumaa, Machi 26.