logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nimefurahi sana kwa ajili ya mtoto wangu-Baba yake Faith azungumza baada ya matokeo ya KCPE

Pia alimshukuru Mungu kwa kumwezesha mwanawe na kuwa bora katika mtihani wa KCPE.

image
na Radio Jambo

Habari15 April 2021 - 13:01

Muhtasari


Faith MUmo azungumza baada ya matokeo ya KCPE

Waziri wa Elimu George Magoha Alhamisi, Aprili 15, ametangaza matokeo ya mtihani wa shule za msingi (KCPE) huko Mtihani House jijini Nairobi

Waziri wa Elimu George Magoha Alhamisi, Aprili 15, ametangaza matokeo ya mtihani wa shule za msingi (KCPE) huko Mtihani House jijini Nairobi.

Wakati wa mkutano na waandishi wa habari, Magoha alibaini kuwa utendaji wa jumla katika 2020 uliboreshwa ikilinganishwa na ile ya 2019.

Mumo Faith kutoka shule ya msingi ya Kari Mwailu aliongoza kwa alama 433, huku akiwa mwanafunzi bora katika mtihani wa KCPE wa mwaka wa 2020.

 
 

Paul Mumo baba yake Faith akizungumza na radiojambo alisema kwamba amefurahi kwa ajili ya mwanawe.

Pia alimshukuru Mungu kwa kumwezesha mwanawe na kuwa bora katika mtihani wa KCPE.

Alikuwa na haya ya kusema;

"Nimefurahi kwa ajili ya Faith, pia namshukuru Mungu kwa kumwezesha, faith ni mwanafunzi na mwana mwema na mwerevu, wakati wa corona tulikuwa tunamuhimiza asome kwa ajili ya mtihani

Ata aliyekuwa mwalimu wake mkuu alikuwa ametuambia kwamba Faith ataongoza katika mtihani wa KCPE," Alisema Mumo.

Pia Faith akizungumza alisema kwamba hakutarajia kuwa ataweza kuongoza katika mtihani wake.

"Nimefurahi sana kwa matokeo yangu, sikutarajia kwamba nitaongoza, lakini nawashukuru wazazi wangu kwa kuniunga mkono,"

 

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved