Wakenya wengi mitandaoni wameonyesha kutoridhishwa kwao na hatua ya serikali ya Kaunti ya Nairobi kupatia barabara jina lake katibu mkuu wa COTU.
Wakenya mitandaoni wameonyesha kutoridhishwa kwao na hatua ya serikali ya Kaunti ya Nairobi kupatia barabara jina lake katibu mkuu wa COTU, Francis Atwoli.
Kaunti ya Nairobi inayoongozwa na Ann Kananu ilibadilisha jina la barabara ya 'Dik Dik Road' iliyoko katika maeneo ya Kileleshwana, Nairobi na kuipa jina mpya 'Francis Atwoli Road'
Huku akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa barabara hiyo, Atwoli alisema kuwa hicho ni kitendo cha heshima sio kwake tu bali pia viongozi wengine wa muungano wa wafanyikazi nchini ambao walioaga.
— Francis Atwoli NOM (DZA), CBS, EBS, MBS. (@AtwoliDza) May 27, 2021
"Ningependa kushukuru uongozi wa kaunti ya Nairobi chini ya Bi Ann Kananu kwa heshima hii na kwa kwa kutambua kazi ya serikali ya leo, jumuiya na wafanyakazi wote. Tutaendelea kushirikiana na uongozi wa kaunti hii" Atwoli aliandika kwenye mtandao wa Twitter.
Hata hivyo, jambo hilo lilionekana kuibua gumzo kubwa mtandaoni huku Wakenya wengi wakionyesha kughadhabishwa na kitendo hicho. Wengi waliachilia jumbe za kukashifu serikali ya Nairobi chini ya ujumbe wa Atoli akipongeza kaunti hiyo huku wengine wakiandika jumbe zao kando.
"Barabara ya Francis Atwoli ni tusi kubwa sana kwa Wakenya" Robert Alai aliandika.
"Ati gavana Ann Kananu amemtunuku Atwoli? Wananchi hawakuhusishwa, naenda kotini, hii haiambatani na sheria, itupiliwe mbali" mtumizi mwingine wa Twitter @kennethnmwiti alisema.
"Amefanyia Wakenya nini haswa? Hakuna chochote cha kuzungumzia baada ya miaka hiyo yote! " @x_stopher aliandika.
Hata hivyo, Wakenya wengine walimpongeza kiongozi huyo ambaye ameongoza COTU kwa kipindi cha miaka ishirini sasa wakisema kuwa alistahili heshima ile.
"Ni muhimu kupongeza Wakenya mashuhuri wakati ambao bado wako hai. Huwa tunangoja miaka baada wametuacha kujifanya vile tuliwapenda. Hongera, Bw Atwoli, umeheshimika vilivyo" @ItsMutai aliandika
"Wakenya wengine waweza kuwa na maoni tofauti lakini Bw Atwoli amefanya COTU kutambulikana nchini. Miungano ya wafanyakazi sio ya watu wenye roho nyepesi, Hongera" @Dr_Mndonye alichapisha.
Hizi hapa baadhi ya hisia za Wakenya katika mtandao wa Twitter.
A Francis Atwoli Road is an insult to Kenyan worker. Huge insult.
— Robert Alai, HSC (@RobertAlai) May 27, 2021
I thought Kileleshwa Residents were good people? What wrong have they done the City to deserve this? So that great girls school - Kenya High - will change their address to "Off Atwoli Road"? It is true - "bad things happen to good people"!...AOL😭😭😭😭😭😡😡😡 pic.twitter.com/eWBkd96kpA
— Prof. Alfred Omenya (@aomenya) May 27, 2021
I thought roads are named after heroes. Why should a road be named after Atwoli? Overstaying in an office doesn't make one a hero or a legend.
— Naibei (@Nai6ei) May 27, 2021
Congratulations Francis Atwoli for having a road named after you. You are an inspiration to corrupt officials. You are prove that undeserved accolades are possible. You are a sign that Kenyan history is a lie. You have shown that eating public money increases weight & govt clout
— Nahashon Kimemia (@nahashon87) May 27, 2021
Some Kenyans might have different opinions from @AtwoliDza But he has given COTU visibility in this country. Trade unions aren't for the faint hearted👊👊 https://t.co/yZG6GP8hdV
— MICHAEL NDONYE 🇰🇪POLITICAL CHESSBOARD📰 (@Dr_Mndonye) May 27, 2021
It's important to honour great Kenyans while they are alive with us right here. Not years after they have gone, so that we be pretending that we adored them. Congratulations Mzee @AtwoliDza. Well honoured. pic.twitter.com/uH7s6CaoSh
— Lord Abraham Mutai (@ItsMutai) May 27, 2021
Congratulations Bazu...your emphatic fights for the workers of this country, their social justice and equality will never go unrecognized. You are the blaze that show the way to trade unionism in Africa...viva! ✊🏾 https://t.co/TWqwAiOJ2u
— Ahmedkadar (@Ahmedkadar1) May 27, 2021
Je, hisia zako ni zipi kuhusiana na uzinduzi wa Barabara ya Atwoli?