logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Buriani, Rais Kenyatta na Ruto wamuomboleza mwakilishi wadi ya Eldas, Ibrahim Abass

Abass aliaga dunia siku ya Jumapili akiwa Wajir baada ya kuugua kwa kipindi kifupi.

image
na Radio Jambo

Habari05 July 2021 - 03:00

Muhtasari


•Rais Kenyatta alimtaja mwakilishi wadi huyo kama kiongozi mwenye maendeleo na ambaye ana uongozi wa mabadiliko.

•Kwa ujumbe wake, naibu rais William Ruto alimtaja kama kiongozi mwenye bidii na maendeleo makubwa. 

MCA Ibrahim Abass

Viongozi wakuu nchini, rais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto wamemuomboleza mjumbe wa wadi  ya Eldas  Ibrahim Abass.

Wawili hao wametuma jumbe za rambi rambi kwa jamaa, marafiki na wakazi wa Eldas baada ya kumpoteza Abass ambaye aliaga kufuatia maradhi ya kipindi kifupi.

Rais Kenyatta alimtaja mwakilishi wadi huyo kama kiongozi mwenye maendeleo na ambaye ana uongozi wa mabadiliko.

"Kuaga kwa Bw Abass ni pigo kubwa kwa wakazi wa wadi ya Edas na kaunti ya Wajir. MCA marehemu alikuwa kiongozi mwenye maendeleo ambaye aliweza kutoa suluhu ya matatizo yaliyowakumba watu ambao aliwakilisha kufuatia uongozi wake bora" Rais alisema.

Kwa ujumbe wake, naibu rais William Ruto alimtaja kama kiongozi mwenye bidii na maendeleo makubwa. 

"Inallilahi wainaillahi raijuun, kwake Allah tulitoka na kwake tutarudi. Rambi rambi zangu kwa familia, marafiki na wakazi wa Eldas kufuatia kifo cha mjumbe Ibrahim Abass.

Abbas  alikuwa mwanasiasa asiye wa kawaida, mwenye bidiii na maendeleo. Tuko nanyi katika nyakati hizi za maombolezi. Pumzika kwa amani" Ruto aliandika.

Abass aliaga dunia siku ya Jumapili akiwa Wajir  baada ya kuugua kwa kipindi kifupi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved