logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Utaenda naye? Mwanamuziki Reuben Kigame kujitosa kwenye kinyang'anyiro cha urais 2022

Kigame amesema kuwa maafisa wa polisi wamemkataza kufanya mkutano wa kuzindua nia yake leo, Julai 7.

image
na Radio Jambo

Habari07 July 2021 - 06:52

Muhtasari


•Kupitia tangazo alilopakia kwenye mtandao wa Twitter  siku ya Jumanne, Kigame ambaye alipoteza  uwezo wake wa kuona alitangaza kuwa angezindua hadharani azma yake ya kuwania kiti hicho leo(Julai 7)  kati ya saa nne asubuhi na saa sita adhuhuri.

•Hata hivyo kwa ujumbe mwingine ambao ameandika Jumatano asubuhi, Kigame amesema kuwa maafisa wa polisi wamemkataza kufanya mkutano wa kuzindua nia yake.

Mwanamuziki Rueben Kigame

Mwanamuziki wa nyimbo za injili Reuben Kigame ameashiria azma yake ya kuwania kiti cha urais nchini Kenya kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka ujao.

Kupitia tangazo alilopakia kwenye mtandao wa Twitter  siku ya Jumanne, Kigame ambaye alipoteza  uwezo wake wa kuona alitangaza kuwa angezindua hadharani azma yake ya kuwania kiti hicho leo(Julai 7)  kati ya saa nne asubuhi na saa sita adhuhuri.

Hata hivyo kwa ujumbe mwingine ambao ameandika Jumatano asubuhi, Kigame amesema kuwa maafisa wa polisi wamemkataza kufanya mkutano wa kuzindua nia yake.

"Mkutano wa kuzindua nia yangu kuwania kiti cha urais umesimamishwa. Polisi wametuarifu kuwa hakufai kuwana mkusanyiko wa watu leo.  Kejeli gani hii kwa uhuru wa kisiasa ambao tulipata miaka 31 iliyopita! Kaeni mkingoja taarifa nyingine. Bado itafanyika leo" Kigame aliandika.

Kigame ambaye alizaliwa mwaka wa 1966 katika kaunti ya Vihiga alikuja kutambulika sana kutokana na wimbo wake 'Enda Nasi' ambao unaendelea kuchezezwa nchini na nje ya mipaka ya Kenya.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved