logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Nataka kumwambia ajisalimishe,'Wazazi wa askari muuaji hatimaye wazungumza

Vitengo kadhaa vya polisi vimewekwa katika hali ya tahadhari kumsaka afisa wa polisi Caroline Kangogo

image
na Radio Jambo

Habari08 July 2021 - 10:49

Muhtasari


  • Wazazi wa askari muuaji hatimaye wazungumza
Mshukiwa wa mauji ya watu wawili Caroline Kangogo

Maafisa wa DCI wamekuwa wakimsaka afisa wa polisi wa kike Caroline Kangogo ambaye anaonekana kuwa kwenye msururu wa mauaji.

Vitengo kadhaa vya polisi vimewekwa katika hali ya tahadhari kumsaka afisa wa polisi Caroline Kangogo, mtuhumiwa wa mauaji ya Konstebo wa Polisi John Ogweno, huko Nakuru.

Hatua ya kuhusisha vikosi zaidi vya polisi kumsaka mshukiwa ilitokana na tukio la pili ambapo afisa huyo anashukiwa kumpiga risasi tena mtu mwingine eno la Juja, karibu kilomita 200 kutoka tukio la kwanza. Jamaa aliyeuawa alitambuliwa kama Peter Ndwiga Njiru, 32.

Caroline amegongwa vichwa vya habari kwa muda sasa, huku wazazi wake wakizunumza wakati wa maombi nyumbani mwao Elgeyo Marakwet baba yake alimsishi mwanawe ajisalimishe kwa polisi kwani anafahamu sheria vyema.

"Nataka kumsihi mwanangu ajisalimishe kwa polisi kwa maana pia naye ni polisi na anajua sheria

Anapaswa kujisalimisha na kuoea serikali silaha," Aliongea Barnaba Kibor.

Mama yake Leah Kangogo ambaye alionekana kusikitishwa na tabia za mwanawe alishindwa na jinsi mwanawe alibadilika licha yake kuwa mzuri na msaidizi katika familia.

"Mtoto wangu haukufanya vyema kuua watu, unapaswa kuja na kusema kama kuna shida,pole kwa familia ya watu ambao waliuawa na mtoto wangu

Ni kifungua mimba wangu na sijui kwanini amebadilika,anapenda watu sana na nimeshtuka tena sana alikuwa anakuja nyumbani," Alisema Leah.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved