logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Matayarisho ya 2022; Mtangazaji Jalang'o ajiunga rasmi na ODM

Miezi miwili iliyopita Jalang'o alitangaza hadharani azma yake kuwania kiti cha ubunge maeneo ya Lang'ata

image
na Radio Jambo

Habari16 July 2021 - 02:17

Muhtasari


•Jalang'o alikabidhiwa cheti cha uanachama na katibu mkuu wa chama hicho, Edwin Sifuna siku ya Alhamisi.

•Kwa sasa kiti hicho kimekaliwa na Nixon Kiprotich Korir wa Jubilee na ambaye ni mwandani mkubwa wa naibu rais William Ruto.

Mtangazaji na mcheshi mashuhuri nchini Felix Odhiambo Odiwour almaarufu kama Jalang'o amejiunga rais na chama cha ODM.

Jalang'o alikabidhiwa cheti cha uanachama na katibu mkuu wa chama hicho, Edwin Sifuna siku ya Alhamisi.

"Mcheshi na mtangazaji wa radio Felix Odhiambo Odiwour almaarufu kama Jalang'o leo hii amejiunga na chama kikubwa zaidi cha kisiasa nchini Kenya. Alikabidhiwa cheti cha uanachama na SG Edwin Sifuna. Tunaendelea kusonga mbele" ODM ilitangaza.

Haya yanajiri huku ikiwa  imesalia mwaka mmoja tu uchaguzi mkuu kufanyika nchini.

Miezi miwili iliyopita Jalang'o alitangaza hadharani azma yake kuwania kiti cha ubunge maeneo ya Lang'ata, Nairobi.

Chama hicho ni maarufu sana katika eneo bunge la Lang'ata kwani hata kinara wake, Raila Odinga alikuwa mbunge pale hapo awali. 

Kwa sasa kiti hicho kimekaliwa na Nixon Kiprotich Korir wa Jubilee na ambaye ni mwandani mkubwa wa naibu rais William Ruto.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved