logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jamaa ajitia kitanzi baada ya kukatazwa kuuza shamba ya familia Muhoroni

Familia ya marehemu ilikuwa imekutana mapema siku ile ili kujaribu kutafuta suluhu ya mzozo uliokuwa ila maafikiano hayakupatikana.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri20 July 2021 - 13:10

Muhtasari


•Joseph Odhiambo Ouma, 23, anaripotiwa kujitia kitanzi akiwa kwa  nyumba ya jirani kufuatia uamuzi huo wa familia.

•Mwili wake ulipatikana Jumapili jioni ukiwa umening'inia kwa nyumba ya jirani ambako alikuwa anafanya kazi kama msimamizi wa nyumba.

WXvImZ-B.jfif

Mwanaume mmoja kutoka Muhoroni  alijitoa uhai siku ya Jumapili baada ya ndugu zake kumzuia kuuza shamba la familia ili kupata leseni ya gari.

Joseph Odhiambo Ouma, 23, anaripotiwa kujitia kitanzi akiwa kwa  nyumba ya jirani kufuatia uamuzi huo wa familia.

Kulingana na kamanda wa kaunti ya Kisumu Samuel Anampiu, familia ya marehemu ilikuwa imekutana mapema siku ile ili kujaribu kutafuta suluhu ya mzozo uliokuwa ila maafikiano hayakupatikana.

Baada ya juhudi za kutafuta maafikiano kugonga mwamba Ouma alitishia kujitoa uhai.

"Aliskika akisema kuwa anaenda kujitoa uhai kwa sababu ndugu zake wamemnyima haki yake ya uridhi" Anampiu alisema.

Mwili wake ulipatikana Jumapili jioni ukiwa umening'inia kwa nyumba ya jirani ambako alikuwa anafanya kazi kama msimamizi wa nyumba.

Upelelezi kuhusiana na kifo hicho umeanza huku mwili wa marehemu ukihifadhiwa katika mochari ya Ahero.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved