- Raila Odinga aomboleza kifo cha Mke wa Mweka Hazina wa Chama cha ODM
Waziri Mkuu wa zamani Raila Odinga ameomboleza kifo cha mke wa mbunge wa zamani Timothy Bosire, Jane Bosire.
Katika taarifa, kiongozi huyo wa ODM aliomba faraja ya Mungu kwa familia ya familia ya aliyekuwa mbunge wa Kitutu Masaba.
"Mama Ida na mimi tunatuma pole zetu za dhati na za dhati kwa Mhe. @TimothyMEBosire kufuatia kufariki kwa mke wako mpendwa Jane Bosire. Kama familia na kama ODM tunasimama nawe wakati huu mgumu. Uko katika maombi yetu. Tunamwomba Mungu Mwenyezi atawapa nguvu, "Raila alisema.
Marehemu alikata roho akipokea matibabu katika hospitali ya Nairobi, haijabainika alikuwa akiugua ugonjwa upi lakini inasemekana amekuwa mgonjwa kwa muda mrefu.
Kifo chake kilitangazwa kupitia mitandao ya kijamii na chama cha ODM Jumanne, Julai 21.
Mama Ida and I send our deepest and heartfelt condolences to Hon. @TimothyMEBosire following the passing of your dear wife Jane Bosire.
— Raila Odinga (@RailaOdinga) July 21, 2021
As a family and as ODM we stand with you during this difficult time. You are in our prayers.
We ask God the Almighty to grant you fortitude.
" Tumehuzunishwa na kifo cha Mama Jane Bosire, mke wa mweka hazina wetu Mheshimiwa Timothy Bosire. Marehemu aliaga dunia Jumanne, Julai 20 akipokea matibabu katika hospitali ya Nairobi. Kama chama tutasimama na familia ya mheshimiwa wakati huu wa huzuni na majonzi na tuomba Mungu aifariji," ODM ilisema.