logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Majambazi 2 wauawa, 4 watoroka na majeraha kwenye makabiliano ya risasi na polisi Eastleigh

Tanki mbili za maji walizokuwa  wanajaribu kupakia kwa gari lao  baada ya kuziiba zilirejeshwa dukani

image
na

Burudani22 July 2021 - 09:05

Muhtasari


•Kulingana na DCI, genge la wezi sita waliokuwa wamejihami kwa bunduki walivamia duka la kuuza vifaa la Jamarat na  kujaribu kuiba wakati maafisa wa polisi walifika na kuzuia uhalifu kuendelea.

•Wawili wao waliaga papo hapo kutokana na majeraha huku wengine wakinusurika kifo na majeraha ya risai mwilini.

Crime scene

Majambazi wawili waliokuwa wamejihami waliuliwa na wengine wanne kutoroka na majeraha ya risasi walipokabiliwa na polisi kwenye jaribio la wizi maeneo ya Eastleigh.

Kulingana na DCI, genge la wezi sita waliokuwa wamejihami kwa bunduki walivamia duka la kuuza vifaa la Jamarat na  kujaribu kuiba wakati maafisa wa polisi walifika na kuzuia uhalifu kuendelea.

Katika harakati ya kujaribu kujinusuru kifungo majambazi hao walikabiliana na maafisa hao kwenye vita ya risasi ila  wakawezwa nguvu. 

Wawili wao waliaga papo hapo kutokana na majeraha huku wengine wakinusurika kifo na majeraha ya risai mwilini.

Bastola iliyokuwa na risasi tatu na chuma ya kung'oa misumari ni baadhi ya vitu vilivyopatikana katika eneo la tukio.

Tanki mbili za maji walizokuwa  wanajaribu kupakia kwa gari lao  baada ya kuziiba zilirejeshwa dukani.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved