Msiniite mheshimiwa,sitagombea kiti chcochote mwaka wa 2022-Boniface Mwangi awaambia wanamitandao

Muhtasari
  • Katika siku chache zilizopita, Boniface Mwangi amehama kutoka Twitter kwenda Instagram kwa kile alichoelezea kama kufurahi na familia, mkewe Hellen Njeri Mwangi na watoto wa watatu  Nate, Naila na Jabu
Boniface Mwangi
Image: Maktaba

Katika siku chache zilizopita, Boniface Mwangi amehama kutoka Twitter kwenda Instagram kwa kile alichoelezea kama kufurahi na familia, mkewe Hellen Njeri Mwangi na watoto wa watatu  Nate, Naila na Jabu.

Walakini, haikuwa safari laini ya kusafiri kwani inaonekana wanamtandao wamemkera Boniface kwa kumwitamheshima ata baada ya kutangaza kwamba amechukua nafasi kutoka kwa siasa.

"Ikiwa utanitumia ujumbe wa moja kwa moja ukiniita 'bwana' aumheshimiwa, nitaufuta. Sikuchaguliwa kamwe kwa hivyo sikupata jina hilo. nilipokuwa nikigombea nilikataa kuitwa jina hilo, "sehemu ya taarifa yake ilisomeka.

Boniface aliendelea kufunua kwamba hatashindania kiti chochote cha kisiasa katika uchaguzi mkuu wa 2022 kwani anachukua mapumziko yanayohitajika kufanya biashara zake na pia kutumia wakati mwingi na familia yake.

"Sita gombea kiti chochote mwaka ujao,niko katika mapumziko ya siasa,nafanya mambo yangu, nilichukua nafasi kwa maana nataka kuwapa watoto wangu ubora wangu

Nilifanya kile niliweza kutumikia nchi yetu na mambo mengine, sasa wacheni nitumie muda wangu na Mama Bear,Nate,Naila na Jabu, wakati huo nitajifunza kudensi," Aliandika Mwangi.