logo

NOW ON AIR

Listen in Live

IPOA yaanza uchunguzi wa kifo cha kijana wa miaka 17 anayedaiwa kupigwa risasi na polisi Huruma

Polisi walisema kuwa marehemu alipatwa na risasi ambayo ilipigwa hewani na afisa mmoja aliyekuwa na nia ya kutawanya kikundi cha raia ambao walikuwa wanawatupia mawe.

image
na Radio Jambo

Habari13 September 2021 - 02:56

Muhtasari


•Maafisa wa IPOA wanatazamia kukusanya ushahidi muhimu kutoka kwa wahusika ikiwemo maafisa wa polisi ili kupata majibu kuhusiana na kifo cha Haila Asanake.

•Polisi walisema kuwa marehemu alipatwa na risasi ambayo ilipigwa hewani na afisa mmoja aliyekuwa na nia ya kutawanya kikundi cha raia ambao walikuwa wanawatupia mawe.

•Mashahidi walidai kwamba  Asanake alikuwa amesimama kwenye roshani ya nyumba yao iliyo kwenye ghorofa ya tatu wakati risasi ilimpata kifuani.

HISANI

Shirika huru la uangalizi wa polisi nchini(IPOA) linachunguza kifo cha kijana wa miaka 17 anayedaiwa kupigwa risasi na mmoja wa maafisa wa polisi ambao walikuwa wanafanya msako wa madawa ya kulevya  katika mtaa wa Huruma, Nairobi mnamo Septemba 8.

Maafisa wa IPOA wanatazamia kukusanya ushahidi muhimu kutoka kwa wahusika ikiwemo maafisa wa polisi ili kupata majibu kuhusiana na kifo cha Haila Asanake.

Upasuaji wa mwili ambao ulifanya kufuatia kifo chake ulidhihirisha kuwa kijana huyo aliangamia kutokana na kuvunja damu nyingi baada ya kupigwa risasi kwenye kifua chake.

Mwenyekiti wa  IPOA Anne Makori amesisitiza kwamba iwapo yeyote atapatikana na hatia shirika hilo halitasita kutoa mapendekezo ya hatua itakayochukuliwa ikiwemo uwezekano wa kushtakiwa.

Polisi walisema kuwa marehemu alipatwa na risasi ambayo ilipigwa hewani na afisa mmoja aliyekuwa na nia ya kutawanya kikundi cha raia ambao walikuwa wanawatupia mawe.

Mashahidi walidai kwamba  Asanake alikuwa amesimama kwenye roshani ya nyumba yao iliyo kwenye ghorofa ya tatu wakati risasi ilimpata kifuani.

Polisi walieleza kuwa walikuwa wamesimamisha gari ambalo walishuku kutumika na muuzaji madawa ya kulevya  mida ya saa kumi na mbili jioni wakati walikabiliwa na upinzani.

Kizaazaa kilianza na kuvutia baadhi ya wakazi ambao walianza kuwatupia maafisa wale mawe na bidhaa zingine.

Hapo wakalazimika kupiga risasi hewani ili kuwafukuza wakazi wale ambao walitaka mshukiwa aachiliwe huru.

Katika harakati hiyo Asanake akapatwa na risasi moja ila maafisa wale walipokuwa wanaondoka hawakufahamu kuwa kuna mtu aliyekuwa amepatwa na risasi yao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved