logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Huwa natandika vitanda vyao kila asubuhi,'Mama ya ndugu 2 waliouawa wa Kianjokoma asema

Benson alikuwa anapenda mambo ya upishi, naye ndugu yake alikuwa anapenda ukulima,

image
na Radio Jambo

Yanayojiri18 September 2021 - 20:30

Muhtasari


  • Wakenya wanaweza kuwa wamesahau kisa hicho na kuendelea na maisha yao  lakini uchungu wa mwana aujuaye ni mzazi
  • Ni takriban miezi miwili tangu ndugu 2 wa Kianjokoma kaunti ya Kiambu kudaiwa kuuawa na polisi masaa ya kafyu
Mandugu wawili wanaodaiwa kufariki mikononi mwa maafisa wa polisi

Wakenya wanaweza kuwa wamesahau kisa hicho na kuendelea na maisha yao, lakini uchungu wa mwana aujuaye ni mzazi.

Ni takriban miezi miwili tangu ndugu 2 wa Kianjokoma kaunti ya Kiambu kudaiwa kuuawa na polisi masaa ya kafyu.

Emanuel na Benson walikuwa wakitoka kazini  kuelekea nyumbani walipokutana na mauti yao.

Mama yao Catherine Wawira, akiwa kwenye mahojiano na TV47, alisema kwamba tangu wanawe waage dunia hajakuwa na nguvu ya kukutana na watu.

"Tangu watoto wangu waage dunia sijawahi wala kusikia kuenda sokoni wala kuhudhuria vyama, lakini tunaachia Mungu

Benson alikuwa anapenda mambo ya upishi, naye ndugu yake alikuwa anapenda ukulima, alikuwa na kuku ambao nilikuwa nawalinda, ni ndugu ambao walikuwa na furaha sana," Alizungumza Catherine.

Kulingana na Catherine walikuwa wamepangana na mume wake wazae watoto wanne, huku akisema hata akiamua kuzaa hawezi kujifungua wanawe ambao waliaga dunia.

"Ata ukiamua kujifungua siwezi jifungua Benson ama Emanuel, huwa napita kwenye vyumba vyao vya kulala kila asubuhi na kutandika vitanda vyao hivi ndivyo huwa nakutana na wanangu ata kama hawayuko."

Catherine anatarajia kupata haki kwa wanawe.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved