logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gavana Waiguru atangaza kutetea kiti chake 2022 kupitia chama cha UDA

Alionekana kukubaliana na wito wao ili kulinda kiti chake kwenye tiketi ya UDA.

image
na Radio Jambo

Burudani22 September 2021 - 14:11

Muhtasari


  • Gavana Waiguru atangaza kutetea kiti chake 2022 kupitia chama cha UDA
Gavana Waiguru akizungumza mwakani 2019

Gavana wa Kirinyaga Anne Waiguru ametoa dalili ya wazi kuwa atatetea kiti chake cha ugavana na tiketi ya chama cha UDA.

Akizungumza na wakazi wa Kirinyaga Jumatano, Waiguru alitangaza nia ya kulinda kiti chake.

Alionekana kukubaliana na wito wao ili kulinda kiti chake kwenye tiketi ya UDA.

Waiguru alikuwa amewaomba umati kama wangeweza kumchagua kama Gavana na waliitikia kwa uthibitisho.

“Nilisema nitafanya vile watu wa Kirinyaga wanataka. Nataka niwaulize mnataka nikuje na chama gani huku Kirinyaga ili mnirudishe? Waiguru aliuliza.

“Nikikuja na hio chama mtanirudisha? Mimi nitasema si mimi nilisema, nimeuliza wananchi na nitafanya vile wanasema,” alisema Waiguru baada ya kuarifiwa ajiunge na UDA.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved