logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanafunzi wa darasa la 7 ajitia kitanzi Siaya baada ya kulalamika kuhusu kupigwa na mwalimu mara kwa mara

Inasemekana kuwa mvulana huyo alifariki alipokuwa anapokea matibabu katika hospitali ya rufaa ya kaunti ya Siaya baada ya wanafamilia kumpata akiwa ananing'inia kwa mti mmoja nyumbani kwao.

image
na Radio Jambo

Habari23 September 2021 - 10:11

Muhtasari


•Inasemekana kuwa mvulana huyo alifariki alipokuwa anapokea matibabu katika hospitali ya rufaa ya kaunti ya Siaya baada ya wanafamilia kumpata akiwa ananing'inia kwa mti mmoja nyumbani kwao.

•Dada ya marehemu, Millicent Onyango alisema kuwa ndugu yake alikuja nyumbani akiwa analalamika kwamba kuna mwalimu alikuwa na mazoea ya kumpiga mara kwa mara. Alisema kuwa alikuwa amechoshwa na kitendo cha mwalimu huyo.

meru

Habari na Philip Onyango (KNA)

Wazazi wa wanafunzi wa shule ya msingi ya Kalenjuok, iliyo eneo la Alego kaunti ya Siaya walishiriki maandamano siku ya Jumatano baada ya mmoja wao kujitia kitanzi kutokana na matatizo shuleni.

Evans Onyango ambaye alikuwa mwanafunzi wa darasa la saba anaripotiwa kujitoa uhai mnamo Jumanne jioni muda mfupi tu baada ya kusikika akilalamika kuhusu kupigwa mara kwa mara na mmoja wa walimu wake.

Inasemekana kuwa mvulana huyo alifariki alipokuwa anapokea matibabu katika hospitali ya rufaa ya kaunti ya Siaya baada ya wanafamilia kumpata akiwa ananing'inia kwa mti mmoja nyumbani kwao.

Dada ya marehemu, Millicent Onyango alisema kuwa ndugu yake alikuja nyumbani akiwa analalamika kwamba kuna mwalimu alikuwa na mazoea ya kumpiga mara kwa mara. Alisema kuwa alikuwa amechoshwa na kitendo cha mwalimu huyo.

Millicent alitoka nyumbani na kuacha ndugu yake akiwa amejawa na ghadhabu na baadae mpwa  wao akamuona kwa mti akiwa amejitia kitanzi.

Habari hizo zilipofika shuleni asubuhi ya Jumatano, wanafunzi na wazazi waliokuwa wamejawa na hasira walishiriki maandamano wakilalamikia mwalimu anayedaiwa kusukuma mwanafunzi huyo afike hatua ya kujitoa uhai.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali ya Siaya huku upasuaji wa mwili ukisubiriwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved