logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mshtuko Nanyuki baada ya vijana wawili kujitia kitanzi

Kesi za watu kujitoa uhai zimekithiri sana katika eneo hilo, kesi mbili za hivi karibuni zikifikisha jumla ya waliojitoa uhai ndani ya wiki moja kuwa watu saba

image
na Radio Jambo

Habari06 October 2021 - 03:00

Muhtasari


•Kesi za watu kujitoa uhai zimekithiri sana katika eneo hilo, kesi mbili za hivi karibuni zikifikisha jumla ya waliojitoa uhai ndani ya wiki moja kuwa watu saba

•Chifu amesihi vijana kufunguka kuhusu masaibu yao kwa marafiki, maafisa na wataalam badala ya kufanya maamuzi ya kujitoa uhai.

meru

Hali ya mshtuko imetanda katika eneo la Nanyuki baada ya vijana wawili kupatikana wakiwa wamejitia kitanzi siku ya Jumatatu.

Alipokuwa anathibitisha matukio hayo, chifu wa Nanyuki Duncan Wachira alisema kuwa jamaa wale walijitoa uhai katika sehemu mbalimbali za mji huo asubuhi ya Jumatatu. Wachira alisema kwamba wawili hao hawakuweza kutambulishwa mara moja.

Mwili mmoja ulipatikana ukiwa umening'inia kwa mti mmoja katika makaburi  ya Waislamu, eneo la Asian Quarters ilhali mwili wa pili ulipatikana ndani ya chumba cha kukodishwa upande wa Thingithu.

Wachira alisema kuwa kesi za watu kujitoa uhai zimekithiri sana katika eneo hilo, kesi mbili za hivi karibuni zikifikisha jumla ya waliojitoa uhai ndani ya wiki moja kuwa watu saba.

"Hawa vijana wote ambao wamejitoa uhai katika kipindi cha wiki moja illiyopita hawajatimia umriwa miaka 35. Inashtua matukio haya kutokea ndani ya wiki moja" Wachira alisema.

Alisema kwamba alipokea simu asubuhi ya Jumatatu kutoka kwa mzee mmoja wa Nyumba Kumi ambaye alimfahamisha kuhusu jamaa ambaye alikuwa amejitoa uhai katika eneo la Asian Quarters. 

Majina ya marehemu hayakutambulishwa kwani familia zao hazikuwa zimefahamishwa. Wawili hao hawakuacha ujumbe wowote kwa hivyo ni ngumu kubaini kilichowachochea kujitoa uhai.

Chifu amesihi vijana kufunguka kuhusu masaibu yao kwa marafiki, maafisa na wataalam badala ya kufanya maamuzi ya kujitoa uhai.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved