logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Seneti yamuita waziri Amina kwa kukosa kufika mbele yake kuhusiana na akaunti za FKF

Walimshutumu Waziri kwa kudharau kamati hiyo, na Bunge kwa ujumla.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri11 November 2021 - 09:13

Muhtasari


  • Seneti yatoa wito kwa waziri Amina kwa kukosa kufika mbele yake kuhusu akaunti za FKF

Kamati ya seneti imemwita waziri wa michezo Amina Mohammed kwa kukosa kufika mbele ya jopo hilo.

Waziri huyo amealikwa kufika mbele ya kamati ya kazi na ustawi wa jamii siku ya Alhamisi kuelezea uamuzi wa kuagiza ukaguzi wa hesabu za FKF.

Hata hivyo, Amina alishindwa kujitokeza.

Badala yake, alituma barua kwa spika Kenneth Lusaka Jumanne, akitaka mkutano huo uahirishwe kwa siku saba.

Katika barua yake, CA ilisema aliratibiwa kupokea ripoti ya ukaguzi wa FKF siku ya Alhamisi kwa hivyo alihitaji muda wa kuchunguza na kuelewa maudhui ya ripoti hiyo kabla ya kufika mbele ya jopo.

“Kwa hiyo itakuwa ni jambo la busara zaidi kuwa na kikao baada ya ripoti kupokelewa rasmi na inaweza kushirikishwa na kamati tukufu,” inasomeka sehemu ya barua hiyo.

Barua hiyo na onyesho la Waziri ilizua hisia kali kutoka kwa wanachama wa kamati inayoongozwa na seneta wa Nairobi Johnson Sakaja.

Walimshutumu Waziri kwa kudharau kamati hiyo, na Bunge kwa ujumla.

"Ninataka kuagiza kama ifuatavyo; wito utolewe kwa Waziri Amina Mohammed kufika mbele ya kamati hii Jumanne saa 10 asubuhi," Sakaja alisema.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved